SMS NZURI ZA MAPENZI SOMA MTUMIE NA UMPENDAE



Najiuliza kila leo hivi ni mimi tu kimeo katika

dunia hii ya leo maana kila leo nayempata

huishia kunipa ahadi kila leo, mpenzi kila siku

waniaidi mara nitakupa leo mara kabla ya

machweo, hivi ni lini utanipa jibu la uhakika

nakunipa mapenzi ya uhakika nipate farijika?

Nakupenda mpenzi.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Hakika mtoto umeumbika mithili ya malaika

japo mbinguni sijafika lakini nauhakika kwa

kila mwanaume aliyeumbika na kukamilika

akikuona lazima udenda utamtoka, naomba

japo yako dakika nipate kukueleza moyoni

yaliyonifika kwani siwezi tena kuficha jinsi

navyokupenda, nakupenda amini kwako

nimefika!

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Nakupenda dear, amini moyoni umeniingia

ndiyo maana mimba nikaamua kukubebea

pasipo kunioa hakika mahaba yako yanifanya

nijione malkia katika hii dunia! Nakupenda

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Ukweli lazima nikwambiye kwa kuwa sina

kimbilio nakupenda kijana mwenzio sijui

kwanini hutaki kukisikia changu kilio,

namwomba Mungu kila kukicha usikiye changu

kilio, nakupenda na kama kukueleza hili

nakukosea nisamehe kwani si langu

kusudio,luv u mwaah.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Mhh kweli wewe ni mtaalam, unayejua

kuitumia yako kalamu kila nikuonapo hupata

hamu, hujihisi kupoteza fahamu, naomba

ufahamu wewe ndio wangu mtaalam!

Nakumiss

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Kweli wewe ni mpishi! Umahiri wako unaanza

kwenye ukunaji nazi hadi upakuaji.

Upekechapo ndizi za mtori mimi huwa hoi.

Nakupenda mpenzi.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Ooh My . . . . Hivi ni kweli umebanwa na kazi

au unaniwekea pozi? Mawasaliano yalikuwa

hayaishi tulipolianza letu penzi, leo si simu

wala sms nizipatazo toka kwako mpenzi,

hakika hunipendi siku hizi, enewei sina jinsi,

zaidi ya kumshukuru mwenyezi!

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Mmh! Nakumbuka siku ya kwanza maneno

matamu uliyoniambia, ahadi kede ulinipatia,

nakunifanya nijione malkia katika hii dunia,

lakini leo umenibadilikia au kukupa penzi

nimekosea?

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Honey hivi unakumbuka? Ahadi uliyonipa,

mwisho wa mwezi ukifika pesa utanipa,

nitatuwe matatizo yaliyonifika, la azizi

nakukumbusha tarehe zimefika, na tatizo

langu bila wewe haliwezi tatulika! Luv u

mwaah.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Mpenzi hakika ningekupa ila tarehe mbaya

zimefika hali ya hewa imechafuka, vumilia

wikiendi ijayo nitakupa, usiwe na pupa, mbivu

zako nitakupa hakuna mwingine wakumpa, luv

u.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Thamani ya Mapenzi yako nikubwa kwangu,

haifanani nachochote kwenye huu ulimwengu,

sina budi kumshukuru mungu, kwa kunijaalia

mpenzi mwema unaejali hisia zangu,

USICHOKE KUNIPENDA MPENZI

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Dhamira kuu ya Moyo wangu ni Mapenzi,

kukupenda kwa dhati bila kipingamizi, kuishi

nawewe kihalali kwa kudra za wazazi, Nipende

nikupende Tudumishe Mapenzi. "NAKUTAKIA

MCHANA MWEMA MPENZI WANGU"

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Kwa kawaida busu la mafanikio hubusiwa

usoni, busu la amani hubusiwa mashavuni,

busu la upendo hubusiwa mdomoni, busu la

mapenzi hubusiwa shingoni, Je wapi nikubusu

ili ulale kwa raha sweet ?

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Naapa abadani penzi langu sitalitoa asilani

ingawa upo mbali nami, nakupenda amini

kwako nimefika, nitunzie langu penzi wasije

niibia washenzi.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Hakikisho la mapenzi: . . umeingia moyoni

mwangu kukutoa itakuwa ngumu sana,wajua

moyo huwa unafunguliwa mara moja hasa kwa

ile true love . . .

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Leo ni zaidi ya mwezi toka tumeyaanza yetu

mapenzi na kila kukicha nakuota kwenye njozi

ukinipa majambozi na huishi uchokozi, sijui

lini nitaacha hizi njozi kwa kunipa laivu lako

penzi, nakupenda mpenzi

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Sijui nini chakukukwambia furaha moyoni kila

saa yanijia tangu ulivyoniambia mimba ndiyo

ishaingia hivyo mtoto nikaye nikimtarajia,

nakupenda dear hakika wewe pekee ndiye

wangu malkia!

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Naamini uatakuwa umerejea kwenye yako

makazi na umechoka na kazi, tafadhali badili

yako mavazi , bafuni ingia upate maji

kujimwagia, natamani kuja kukusaidia mgongo

kuusugua na chakula kukuandalia lakini siku

haijawadia, nakupenda dear!

Comments

Popular posts from this blog

HIZI HAPA SMS TAMU ZA❤️ KUMTAKIA USIKU MWEMA MPENZI WAKO❤️

Maneno mazuri ya Usiku mwema

SMS ZA MAPENZI ZENYE UJUMBE MTAMU KWA MPENZI WAKO